Naipenda Jumamosi yangu - Stori bomba ya uhusiano - Chumba Cha Mapenzi -->

Naipenda Jumamosi yangu - Stori bomba ya uhusiano

Salamu kwenu wote
Eid Mubarak
Leo sikukuu tena, hakuna kulala usiku/asubuhi hii nipo natoka Msondo Ngoma.

Inasumuliwa na Irene Mbowe. (Inaanzia sehemu ya kwanza na kuendelea, fatilia uhondo moto moto. Jadili hadi uchoke kumekucha.

********************************
fb_img_1559779778596-jpg.1119084


SHUHUDA NAIPENDA JUMAMOSI YANGU.
Shikamoo dada Irene.
Naomba na mimi nitoe shuhuda yangu juu ya Naipenda Jumamosi yangu.
Naitwa Marino. Ni mama na Mke. Nina watoto 3.
Niliolewa mwaka 2009. Nina ndoa ya miaka 10 sasa.
Nimeishi ndoa ya mateso na masumango sana kwa muda mrefu. Nimekuwa nikilia kwa takfibani miaka yote .Mpaka siku moja mwaka 2015 nilipoambiwa nikufollow. Nilianza kukufolow na sikuona kitu cha kunisaidia wakati huo. Nilikuwa nakusoma lakini sikuona kitu cha kumisaidia.
Nafikiri ni kwa sababu moyo wangu ulikuwa na uchungu na majeraha.
Irene Unaolewa ukiamini kabisa una mwenza wa ndoa ambaye atakuwa na wewe. Lakini ajabu ni kwamba unakuwa na Adui ndani ya nyumba.
Lakini hata hivyo unajipa moyo kwa ule usemi usemao ,
ukiona kwako kunaungua kwa mwenzako kuna teketea. Ni usemi ambao najifariji nao.
Lakini kuna uwezekano kwa we.zako ndiko kuna ungua kwako kunateketea. Ninawaza hayo.
Siku zinazidi kusonga bila mafanikio yoyote.
Kila unagejaribu kumwambia juu ya Ndoa yako na matatizo anakupa majibu.
Nakumbuka sasa nikaona aliyeniambia msome Irene Mbowe nimamuona hafai na nikaachana na kusoma.
Ni siku ya jumapili nakutana na Mama Karisa. Namuambia juu ya Ndoa yangu na Kuamwambia juu ya Kumsoma Irene Mbowe.
MamaKarisa anatabasamu kisha anaachia cheko refu na kusema Huyo Irene Mbowe yeye ndoa yake salama ama?
Anaongea kwa kumaanisha sana. Na Ili kunivunja moyo kabisa Akaniambia,Irene Mbowe mwenyewe ndoa imemshindaga kitambo ni mfamaji na Mume aliye naye sio mumewe ila alichukua mume wa mtu. Kalava baho. Bwana aliyenaye ni mume wa Mtu. Ama hujui makungwi wanaongoza kuachika?
mh...Nimahisi kama kweli. Maana mama Karisa anaongea kwa kumaanisha na kuonyesha Anachokiongea ni kweli.
Nikamuamini sana kutokana na kusisitiza kwake.
Lakini kweli.. Makungwi ni wanawake wa ndoa nyingi.
Lakini kweli, Makungwi wengi wanaachika na hawana ndoa.
Bila shaka huyu Irene naye ni Muhanga na ndio maana ndoa ikamshinda na.sasa ako na mume mwingine.
Sasa Naamini hili na halina ubishi. Naamua kuachana na Kinamkera Irene Mbowe.

Sasa nafanyaje?Namhoji Mama Karisa.
Anisaidie Kupata majibu ya Ndoa yangu.

Sikia mwanamke,Amka usingizini. Ndoa ili idumuazima ujiongeze. Kama mume anakunywa bia kunywa whyski. Kama anakunywa whyski kunywa bia.
Akicheua bia cheua wine,Lazima ndoa iwe nzurii
Mama Karisa anatabasamu na kunitazama.Huku anabana nywele zake vyema. Na Kuniambia mimi natoka.
Ni majira ya mchana kuelekea saa tisa. Namtazama akiwa anatembea kutoka nje . Nami nasimama kutoka nje kumfuata.
Nabakije ndani kwa mtu?
Dadaaaa... Mama Karisa Anaita, Mshefa akija mwambje na mimi ndo nimetoka. Yani muda Naoingia mwambie mmepishana na mama. Sawa?
Mama Karisa anamaliza kumpatia Maelezo Msichana wake wa kazi yani House geli.

Mama,Lakini Karisa Ana moto na Ana jipu mama.
Msichana anatoa maelezo.
Mama Karisa Bila Kujali anasema,Mpe panado moja akiamka.
Kisha ananiambia twende mama.

Namfuata nje na Anaongea na Simu nikiwa nasikia.
...Sema mpenzi... Ndio nakuja hivyo.
Mama karisa anaongea kimahaba.
Mh...Hapa anaongea tu na mwanamume.
Anakata simu na kuitisha Taksii.
Baada ya Muda Taksii inafika na Ananiambia, Nisindikize.
Kwa vile sikuwa napa kwenda naamua kumsindikiza.
Haooo mpaka tunafika Mjini . Anaelekezwa mahali pa kukutana. Tunachukua Taksii ingine haoo tunaanza safari kuelekea Sakina.
Tunafika sakina kituo cha mafuta tunashuka hapo na baada ya dakika chache Inakuja gari ya landcru
user zitumikazo kubebea watalii na ndani kuna mwanaume mmoja tunamsalimia kisha mwanaume huyo anamkumbatia mama Karisa na kumpiga kibao cha makalio kisha tunapanda haoo tunaondoka.
Tunaingia ndani ndani na kukuta Bar moja iko ucho joroni sana.
Tunakuta watu lakini sura ngeni. Ni Bar iliyo changamka sana.
Tunakaa hapo na kuanza kunywa.
Mimi sio mnywaji kabisa. huwa naonja tuu .
Nikaagiza Savanna yangu nikaanza kunywa.
Wakati nakunywa mama Karisa akaniambia wanakuja.
Nikabaki peke yangu. Ni saa kumi na mbili jioni.
Walikaa hasa. Sijui walipokuwa lakini nilijua tuu wako sehemu Wanadinyana. Waliporudi dalili zote za Kutoka kudinyana niliziona. Na walikuwa wamejiachia sana.
Nilikuwa natafakari mambo mengi.
Mama karisa anaonekana mwenye Raha sana. Mume wake namfahamu amezaana mwanamke mmoja. Lakini mama Karisa haonekani kusononeka japo anajua.
Ahaaaa... anapakuburudisha moyo wake.

Natafakari nikiwa pale. Kisha simu yangu inaita. Ni saa moja usiku. Ni Mr anapiga. Niliitazama nikasema uwiii,
Mama Karisa akiwa kalewa akamiambia uwii nini?Akanipokonya simu na Kuizima.Kisha akaniambia Tulia wacha kujitesa. Yeye kamaliza yake ndo anakutafuta?Kashamalizana na.wanawake zake hukoo ndo anakutafuta saaa hizi?Mchana wote mbona asikupigie kama anajali kweli?
Mama karisa alikuwa anaongea kilevi.
Nilikuwa naogopa sana. Sijazoea kukaa nje usiku.
Nikamuomba simu nipige.Akaniambia,Sikia,Kama vipi nikuitie Taxi.
Nilikuwa naogopa.
Sikuwa na amani Tena.

Diaa,Mama karisa alimtazama yule mwanaume na kumuita Diaa,Kisha akamwambiaNaomba tumrush huyu mwanafunzi Hapo aende maana ishakuwa msala.

Yule mwanaume akiwa kamkumbatia Mama karisa akamwambia, Diaa nina hamu sana na wewe. Wacha nimuombe Fadhili ampeleke.
Sawa. Mama Karisa aliitika.
Fadhili akaitwa kisha nimaondoka
kwa gari ile ya Utalii.
Ni saa tatu usiku .Niliwasha simu yangu na hapo hapo zikaingia msg nyingi sana. Ni za mr.Msg ya m
kwanza ilisema,
NITAKUUA LEO. MALAYA MKUBWA WEWE. BAKI HUKO HUKO.
Msg ingine, ikasema,
Wewe malaya unaniximia simu?
Kwangu leo usiingie
Utakuta mabegi yako nje.
Uko wapi wewe Mmbwa?
MUNGU WANGU! Nifanyeje?
Moyo ukanipasuka paaaa.
Dereva akaniangalia akasema,
Mamii mbona kama una mashaka sana?Aluliza..
Nilianza tuu kulia.
savanna 5 nilizokunywa zikayeyuka zoote.
Uwiiiii.
Nishushe hapa,Nishushe.Niliomba kushushwa.
Ni kama nusu km kutoka niliposhushwa mpaka nyumbani.
Nisijue Mr ananiona nikkshushwa.
Akajikausha misijue.
Nikawa nakazana ajabu kutembea. kama nahisi nipae.
Nikafika nyumbani. nikaingia ndani na kuchukua mswaki kwanza.

ITAENDELEA SEHEMU YA PILI. (Post #2)