Naipenda Jumamosi yangu - Stori bomba ya uhusiano - Chumba Cha Mapenzi -->

Naipenda Jumamosi yangu - Stori bomba ya uhusiano

fb_img_1559779817977-jpg.1119086


Nikiwa sina hili wala lile,Nilisbtuliza mlango wa chumbani unabamizwa kwa nguvu,Mungu wangu nilinisemea.
Baba Davis hakuwa na mswalie Mtume.
Moja kwa moja alinifuata bafuni na Kunivitia nje,Kabla sijakaa sawa nikiwa nashangaa alinirushia mabao ya mfululizo,Huku akionekana mwenye hasira sana.
Niambie kwa nini ulizima simu na kwa nini hukupokea simu yangu na ulikuwa wapi na ni nani alikuleta akakushusha njiani,
Ni maswali mengi kwa wakati mmoja.
Maswali yote nina majibu yake. Lakini naanzia wapi kumjibu,Utaniua Bana Davis,Utaniua mume wangu.
Ndio nitakuua... Umalaya umeanza lini?
Hapo alishachukua mkanda wa suruali na ananichapa nao.
Uwii nakufa,Unankumiza baba Davis.
Nalia kwa nguvu na Kafunga mlango wa chumbani. Nilikuwa napata maumivu sana.
Baba Davis nanipiga hivi,kweli?'Yeye akirudi saa tisa usiku nani anampiga?Yeye akilala nje nani anampiga?

Nilikuwa nimekaa chini sakafuni nikiwa nawaza nimjibu nini. Niambie aliyekuleta na kumushusha pale kona ni nani?
Sijaja na mtu,Nilikuwa nimepanda Toyo. Nilimjibu bila kujua aliniona. Nikamwambia nimepanda toyo.. Na nikaapa kabisa.
Mh... aliguna na kuniambia,bado sijakupiga. Utaniambia ukweli leo.
Sasa amua ,Unamtaja aliyekuleta ama Unaondoka?
Wacha niondoke,Wacha niondoke.
Alinyanyua mkanda kwa hasira akanichapa nao rwaachu.. bahati mbaya bakoli ikanivonga puani damu zikaanza kutoka.
Ndipo akaogopa na Kuniacha.
Akatoka nje akawasha gari huyoo.
Hapo ni saa sita usiku.
Nilijiangalia kwenye kiyooo nilivyovimba,animeumia na kuvilia damu hasaa. Nililia sana.
Wakati huo dada na Watoto wamejifungia woote chumbani wako kimya.
Nianzie wapi?Huyu akirudi anarudije?Si atanipiga zaidi?
Niliwaza haraka na nikasema wacha nifuate simu yangu ili nipige kwa Mamdogo wangu.
Nilifuata simu yangu na kuchukua kisha nikapiga kwa mamdogo kumwambia naenda kwake maana nimepigwa sana. Ama la basi aje.
Mamdogo alishtuka maana nilipiga picha madamu yalivyonitapakaaa.
Baada ya Lisaa limoja mamdogo alifika kwangu. Sijui alipata wapi usafiri lakini alitoka Bomang'ombe mpaka Kimandolu ndani ya Lisaa limoja tuuu.
Geti liligongwa na nilishangaa ni mama mdogo.
Mungu wangu,Mama Davis?Mbona umeumia hivyo?Nilikuwa nimevimba sana. Mwili mzima kwa alama za mikanda.
Mamdogo akanibeba na gari aliyokuja nayo hadi hospital. Kufika huko wakatukataa wakasema mpaka PF3,Ikabidi nikatae maana sikuwa nataka kesi. Mamdogo akasema noo. Lazima maana hutatibiwa. Mwisho nikakubali nikaandika maelezo tukapata PF3 Na kwenda kupata matibabu. Baada ya kutibiwa nikaambiwa lazima nilale hospital.
Nikalala na mamdogo.
Yule.dereva akalala guest.
Huku nyuma baba Davis alienda nyumbani akiwa kalewa sana na akalala. Binti wa kazi aliniambia.
Asbh sana Mr akiwa anaelekea kazini alimamatwa na mapolisi kwakosa la akunipiga.Akapelekwa lokapu akafungiwa huko.
Nikiwa hospital mama mkwe akaniandikia msg na akaniambia, "Umalaya wako ndio unasababisha mwanangu ateseke"
Nilishangaa sana mamaanakuwaje hivyo. Kwa nini atumie lugha hiyo mapema kiasi kile. Bila kunipa pole na kutaka kujua kilikoni
*******************
Mume alikamatwa na kuwekwa kituoni. Bado nilikuwa hospital. Saa tisa jioni nikaruhusiwa kutoka. Nikatoka Nikapita nyumbani kuchukua nguo na vitu vya muhimu. Kisha huyoo kwa mama mdogo. Wakati huo mume yuko polisi. Anashukiliwa huko. Alilala lokapu siku tatu bila huruma kabisa.
Mama yake ndiye aliyekuja na akawa akimhudumia. Na baada ya hapo ikabidi nirudi na kikao kikae ya kwamba tupatane. Tukapatakana. Lakini moyoni nina jeraha kubwa sana. Ni kama nina kidonda ambacho hakijapona kabisa. Maumivu niliyokuwa nayo hayakuwa ya kawaida.
Mama Karisa nilimuelezea kila kitu juu ya kipondo kile. Alisikitika sana. Na aliniambia nisijali kila kitu kitakwisha. Aliniambia nivumilie kwa muda mambo yatakuwa shwari.
Niliporudi safari hii Mama Karisa akawa rafiki mkubwa na wa karibu sana. Na akaniambia unashutumiwa kwa kosa ambalo hujafanya.
Mama Karisa aliniambia nakosa mapenzi na upendo.
Akaniambia wako wanaume wenye kujua kupenda na kubembeleza mwanamke. Si kama Baba Davis ambaye ana.roho ya kinyama. Nikaona ni kweli. Kwa sababu mama Karisa ninaahuhudia jinsi anavyopendwa na yule baba.
Mh... Nitapata wapi mpenzi?Nawaza. Baba Davis anajidai mjanja sana. Nitamnyoosha. Niliwaza akilini.
Anafikiri kuwa na mahusiano lazima kurudi usiku eeee. Hanijui. Sasa nitarudi saa kumi jioni na nitakuwa na mpenzi.
Nilianza kutamani kuwa na mpanzi. Kweli ukitembea na fisi unakuwa fisi.
Siku ile nilipotoka pale Bar Fadhili alinidrive mpaka kona. Alikuwa akiniambia ananipenda. mh.
Simjui vizuri lakini ni mwanaume ambaye nilitamani sasa kuwa naye.
Mama Karisa asijue nawaza nini akilini akaniambia,Hivi unajua Fadhili anakupenda sana?
Hivi unajua nilimwambia umepigwa kwa ajili yake akasikitika sana?Ni vile alisema hatakupigia simu anataka kukuona ana kwa ana.Unaonaje nikimwambia mkutane?
Sawa kabisa. Tena mwambie anipigie.
Nilijibu haraka sanaNa swntensi hiyo nikaisindikiza na maneno,
Ukiona wa nini wenzako wanasema tutakipata lini... Nilisema kwa hasira.
Mama Karisa akacheka, Ha ha ha... Ayeya... Asusa... Kisha akanigongea kunipa Tano.
Alipimaliza kucheka akapiga simu na kumwambia aliyempigia,
Kazi ni kwako,Ushindwe mwenyewe...Nikajua alikuwa akimpigia Fadhili.
Baada ya dakika mbili nilipigiwa simu. Mama Karisa akaitazama simu yangu akaniambia,Fadhili huyoo.
Pokea. Nilipokea,
Haloo Mwanamke unayeninyima usingizi...... Alisema Fadhili.
Maneno hayo yalipenya moyoni vaap... Nikasikia faraja na burudiko. Nikaachia tabasamu.
Sema.. Nikajibu huku Natabasamu.
Nakupenda sana wewe mwanamke. Nashukuru Mungu kukutana na wewe. Tangu nikuone ile siku mpaka leo Nateseka. Lakini nafurahia mateso haya kwa sababu ni ya Mapenzi. Tangu nimezaliwa nimegundua sijawahi kuteswa na mapenzi kiasi hiki. I love you mamiii. Nakuoenda. Wewe ni mtu mzima najua unaelewa nini maana ya Kupenda.

Dah... Maneno hayo yananifanya nakuwa kama mjinga kabisa.
Natabasamu kisha namwambia, 
Na weweee....
Ndio mamii namaanisha. Na hivi leo nimesikia sauti yako ndio kabisaaaa... Sijui kama Nitalala. Ila napenda ninavyoteseka juu yako. Fadhili aliendelea.Kisha akaniambia tena kabla hajakata simu,
NAOMBA NIKUONE KAMA HUTAJALI. KISHA UNIJIBU KAMA UNANIPENDA AMA LA.
Alimaliza kuongea. Nikamtazama Mama Karisa ambaye naye alikuwa akinitazama.
Akaniambia enhee... Sema. Mwanaume ndo huyo. Namjua Fadhili. Anajua kupenda sana. Na ana care ile mbaya. Mwanaume hasaaa.
Kasemaje?Mama Karisa aliniuliza.
Mh... Niliguna... Mama Karisa akaniambia,Waacha weee....
Nikamwambia, Hivi Hana mke?
Mama Karisa akacheka sana.
Una nini wewe?Kwani Mke Ndo nini?Wewe Huna Mume kwani?
Unataka ndoa unataka mapenzi?Hata angakuwa nao kumi,What you need is Love. Full stop. Hembu kua bwana na wewe.
Mama karisa aliniambia.
Bado nilitamani kujua juu ya Fadhili.
Mama Karisa acha utani Bana. Fadhili hana Mke?
Mama Karisa alinitazama sasa hivi akiwa serious kidogo.
Mke anaye na watoto 2. Lakini haihusiani na Mapenzi yako na yeye. Unahitaji faraja ya moyo. Unahitaji Mapenzi. Full stop. Hata angekuwa na wake sita ni wakwake. Wewe pata mapenzi urudi ukaleee wanao. Ama unataka Ndoa?Mama Karisa akacheka tena.
Mh. Nikasema na kweli.
Wakati huo huo nikachukua simu yangu na kumpigia Fadhili.
Alipokea haraka sana na kuniambia Enhe,Sema kimwana.
Nikajiskia rahaa sana. Sina usemi. Nikajibu.
Akaniambia Nakupenda.
Nikamwambia Asante.Kisha akaniambia enhe... Poza moyo wangu basi. Niambie jambo nijiskie na mimi ni mwanaume.
Alisema kisha nikamwambia Nakupenda pia.
Asante sana. Natoka mazoezi sasa hivi. Naomba nikuambie mahali pa kukutana. Natamani kukuona mpenzi.
Fadhili aliniambia hivyo.
Uwii. Mama Karisa alinitazama akaniambia,Haya mwali. Kazi ni kwako. Mimi nikuache. Take care. Ushindwe mwenyeww. Bwana ndo huyo. Janaume la miraba sita, Ana kazi nzuri sana. Ana pesa na Anajua mapenzi. Ukikosa raha tena usinililie. Alafu tabia ya kila ukikutana na mimi unalia lia ooo ndoa ndoa,koma. Ukikutana na mimi nataka kusikia mambo ya malavi davi. Sawa bibi?Upo?Baiii... Take care.
Mama Karisa aliondoka akaniacha nimeduwaa.
Baada ya li saa Fadhili akanipigia simu na kunielekeza pa kumkuta. Akaniambia anamtuma na.dereva kabisa nitembee mpaka mahali kona kisha dereva wake atanichukua hapo.
Nilijivalisha nguo haraka huyooo. Nikaondoka.
Nilifika aliposema atatuma Dereva na kweli nikamkuta.Kisha Dereva huyo akaendesha gari mpaka kwenye Ile.ile Bar. Nikafika. Akanikumbatia kama mtu ambaye tulishaonana. Nilikuwa na.hofu sana. Akaniambia unaonekana unaogopa sana.
Tuhame hapa tuhamie ndani?Ndio. Nilijibu.
Wakati huo dakika chache simu yangu ikaita.Ni Mr alikuwa anapiga. Moyo ukapasuka paaa. Fadhili akanitazama na kuniambia maskini,Utakufa,Huyu mwanaume anakufanyaga nini?Hembu usipokee hiyo simu. Wacha iite mpaka izime. Usipokeee. Sitaki kabisa kuona unakosa raha.
Sikia Mamii, Ukitaka kula nguruwe chagua aliyenona.
Hivi Diaa unajua na mimi nina mke ila kwako moyo wangu umefika?Si unaona simu yangu nimeweka kabisa silencer?Nataka kufaidi penzi lako. Sasa sikia, kama unataka tufaidiane hawa wenzetu wakae pembeni. Sawa?Ili sisi tufurahie mapenzi . Sawa eee. Usijali nitakufunindisha kila kitu usiogope.
Bado akili yangu ilikuwa kwenye Simu ya Mr.
Fadhili aliniambia Nakupenda Dia. Naona huyo Hitla wako anakukosesha Raha. Unaonaje nimuite Dereva akurudishe kwanza kisha tutaonana ukiwa umetulia?
Moyoni nikasema mh... Mara nimkose Fadhili itakuwaje?Nikajiambia liwalo na liwe. Wacha ni kubali tuu. Nikachukua simu nikaandika niko Salon.
Basi nikatuma msg.Fadhili akaniangalia akasema Asante kunipenda. Unadanganya kwa ajili yangu sitakuangusha. Nitakupa mapenzi kuonyesha najali na unaniheshimu. Jiandae kupendwa.
Dah. Ni kweli ni mama wa miaka 29 wakati huo .Sijawahi kukutana na aina hii ya mwanaume tangu. Nikishangaa sana. Akili yangu ikaniambia kweli penye wajenzi hakuna miti. Mke wake yuko wapi mume anachepuka?
Fadhili aliagiza chakula na Akanilisha. Kwa kunihurumia sana na majeraha yangu maana bado nilikuwa na makovu mwilini. Alisikitika sana kuona nilivyovilia damu.
Tulikula tukamaliza. Kisha akaniambia sitaki upigwe tena. Nenda mamii. Nakupenda. Akinikumbatia kwenye likifua lake la haja. Kama dakika tano hivi. Huku ananiambia ananipenda sana. Mimi ni mrembo sana na atahakikisha Thamani yangu ya kike inarejea.
Mamii,Nataka ujue wewe ni wa Thamani. Nitakupenda mpaka ujue thamani ya Kike maishani. Nataka nikupende ukiwa unatembea kila anayekuona ajue unapendeka. Nataka nikupende mpaka mumeo ajue Unapendwa ila asijue ni nani anakupenda.
Take care...Nakupenda. Nilijikuta nalia sana. Akanibembeleza na kuniambia Nyamaza. Am here for you Diaaa.Tukaagana. Nikawa nasimama kuondoka. Nikapiga hatua kama Tano hivi. Akaniita, Mamii,Mamii Nikageuka Akaniambia nisubiri. Akatembea haraka kunifikia. Akanikumbatia. Kulikuwa na walevi wengine hapo wanakunywa pombe zao wakatuona wakapiga kelele,Weweeee.. weee..Nikaogopa sana. Akaniambia usijali. Washkaji hawa. Kisha akaniambia naomba nikupe pesa. Naomba tuuu. Nikamwambia nooo...Akaniambia naomba nikupe. Akaingiza mkono kwa suruali. Akatoa walet yake. Akahesabu noti za elfu kumi kumi kama noti kumi na tatu. Akanipa. Akaniambia bai.
Nikamwambia Asante. Huyooo nikaenda Home.
Nukafika home saa Tisa mchana. Nikajisemea moyoni waooo. This is love.
Jamani mwanaume yule. uwiii.
Nikachukua Simu yangu nikampigia Kumuambia Nimefika home Salama.
Akaniambia Where is Hitla?Nikacheka. Nikamwambia hajafika bado. Akaniambia poa.Take good care of ur self.
Nikatamani kumsimulia mtu juu ya mapenzi niluyopata.Mapenzi ya maneno. Nikaona isiwe taabu. Nikampigia Mama Karisa. Akapokea. Nikasimulia kuanzia a to z. Akaniambia waoo. Bora shoga angu na.wewe upate raha. Maana dah. Ungekufa na kihoro. Huyo ndo Fadhili mamiii. Mwanaume yule hajawahi kupata mapenzi. Na anajua kupenda. Sasa zubaa uliwe. Na wewe Changamka. Mpende mpendane. All the best mamii. Kama una raha na mimi nina Raha. Ukifurahi ndo raha yangu.

ITAENDELEA SEHEMU YA TATU (post #6)