NAIPENDA JUMAMOSI YANGU SEHEMU YA 4 - Chumba Cha Mapenzi -->

NAIPENDA JUMAMOSI YANGU SEHEMU YA 4

fb_img_1559779857905-jpg.1119134


Nilitamani sana kumjua vyema Fadhili. Ni mwanaume kijana,kama anazidi miaka 35 ni bahati. Lakini anawezaje kumiliki lodge kubwa kiasi hiki?Lakini mke wake yupo wapi?mbona hii nyumba nzuri hivi haiishi mtu?Tena nilipokuwa nakagua haraka haraka sioni kama ni nyumba ambayo mwanamke anaweza kuwepo hapo. Si pachafu lakini hapana usafi wa kuonyesha mwanamke yupo hapo. Nilimtazama Fadhili usoni nikamwambia, Navutiwa na wewe sana.
Aliniambia Karibu. Kisha akanishika mkono na Kunitembez taratibu hadi kqenye balcon kwa nnje. Hapo kuna viti viwili tukakaa. Na meza nzuri tuu. Akaniambia You know what mamii,Hii ni maneja house. Hapa atakaa meneja wa lodge.yetu.
Ahaaa,Nikajibu.
Aliniambia nina hamu sana na unachotaka kuniuliza, enhe.. endelea mama yangu
Aliniambia kisha nikakohoa kidogo kama ninayetengeneza sauti. Kisha nikamwambia,
Kama nitakuwa navuka mipaka nisamehe,Ila natamani sana kujua juu ya Familia yako.
Akinitazama na kuniambia unataka kujua nini hasa mama yangu?Aliongea kwa upole sana.kisha akaniambia,Unafikiri nikikuambia huajiskia vibaya?
Hapana,Sitajiskia vibaya,Niambie tuu.
Okay. Alichukua simu yake na baada ya hapo akaifungua na kunipatia. Akaniambia angalia hizi picha hapa. Nakuja.
Alisimama na kuelekea ndani.
Kisha akarudi na glasi mkono wa kushoto na mkono wa kulia kashikilia chupa ya pombe kali.NiJackdaniel hiyo. Nikumiminie kidogo mama?
Ops.. sorry unatumia dawa bado eee...
Ngoja nije just a moment,Wacha nikuletee vitu laini kama wewe.
Aliondoka na kurudi tena na chupa ya soda ya fanta na glass. Kisha akanimimini na kunipatia Na sasa hivi hakukaa kwenye kiti bali alikaa chini kabisa na kukunja miguu yake kama anayekula pilau la idi.
Kisha akanitazama. Akaniambia umeona hizo picha eee.
Huyo ni mke wangu na hao ni watoto wetu. Nina watoto 4. Na Huyo ndo mke wangu.
Enhe,Kingine mama?
Aliniuliza.
Sikuwa na haraka. Niliona picha nzuri sana za mwabamke mrembo sana. Yani mwanamke mzuri. Mimi ni mwnamke na.tumezoea mwanaume akichepuka ana mke hohe hahe. Lakini sio kwa mwanamke huyo niliyemuona kwa simu. Ni mrembo hasa. Na watoto wazuri wenye furaha.
Kidogo nikama napoteza pozi. Maana mke mke hasa. Sasa kakosa nini huyu mwanaumw jamani?Akili kama zinarudi fulani hivi.
Mamii mbona kama hujaniuliz kitu. Kingine ni nini mama?
Hapana. Asante. Una mke mzuri sana.
Nilimwambia.
Asante. Ila hakufikii hata kodogo. Wewe mzuri sana. Napenda umbo lako,rangi yako,sura yako na sasa nina raha kwa sababu nategemea na Penzi lako nilipende.Fadhili aliniambia. Na kisha akasimama na kuniambia mamii muda muda. Nikitazama simu yangu ni saa kumi na.nusu jioni.
Akaniambia dah.. Yani wewe mwanamke ninavyopenda mazoezi lakini naacha kwa ajili yako. Dah. Nakupenda sana. Aliniambia enhe... Niambie lini utakuwa na nafasi ya siku nzima. Nataka kukaa na.wewe siku nxima. Unipikie,Unilishe,uniogeshe Niambie lini mamiii.
Nilitabasamu nikamwambia hata kesho.
Akacheka. Akaniambia serious?
Yes. I mean it. Nilimkahkikishia ninachokisema nakimaanisha.
Basi sawa kabisa.
Basi naomba nikuwahishe mama yangu. Alafu kesho saa nne tukutane hapa kwa raha zetu. Akitabasamu na kuninyanyua. Kisha tukatoka kuelekea kwenye gari.
Akaniambia niendeshe mpaka pale njia panda kisha Dogo aje kukupick pale.
Sijui kuendesha gari. Nilimjibu.
What?Yes. Sijui kuendesha gari.
Nilirudia tena.
Aiseee.. Mwanamke mzuri hivi hujui kuendesha gari?why?
Nilitabasamu na kusema wacha nichomekeeee. Nikamwambia Mwalimu natoa wapi pesa ya gari?
Akanitazama akatabasamu. Kisha akasema hembu ngoja .Akashika simu yake akabonyeza bonyeza na kuniambia Nikikupa gari utasemaje kwa Hitla wako?
Nilinyamaza dakika moja tu na kumwambia nitamwambia nimekopa. Uwii. Nitafurahi sana sana.Akaniambia basi anza shule,Ila noooo. ..Nitakufundisha mwenyewe. Nitakufundisha peke yangu. Nakupenda sana wewe mwanamke. Nilikuwa nakung'atia tu meno.
Tulifika njia panda. Dogo alinichukua na kunipeleka mpaka anaponishusha siku zoote.Nilishuka na kutembea na mguu hadi nyumbani.
Nilifika nyumbani Mr alikuwa hajafika bado.
Niliandaa chakula na baadae nikala na watoto na kwenda kitandani.
Nilikuwa nogopa sana kupiga simu kwa Fadhili kwani nikiogopa mke wake lakini pia niliogopa Baba Davis asije akafumania msg ataniua.
Hivyo sikuwa na tabia ya kuandika msg. Lakini nikaona wacha nimsimulie mama Karisa .Saa nne nikaanza kuongea na mama Karisa nikampa umbea woote. Akacheka sana na kuniambia bado. Utafurahi sana. Namjua Fadhili ni Alwatani wa mapenzi. Pale umefika mamii. shida ya ndoa yako imeisha. Na ndio sasa usiache kumjali mumeo. Mimi nimeishi na Mpenzi wangu mwaka wa saba huu na mr hajui kabisa. kazi ni kwako. Sawa mamiii. Sawa mrs Fadhili... Kisha akaachia cheko, ha ha ha.... Hongera nyonda.
Alisema hivyo na tukaagana.
Dah. Kupendwa raha sana.
Saa nane mr hajafika. Saa tisa, Mara asbh hii hapa.
Hajafika.
Nikachukia sana. Nikajiandaa na kuelekea kazini. Lakini lengo ni ifike saa nne tukakutane na Fadhili.
Tukikubaliana saa nne. Nilimpigia simu nikaanza kulia nikimuelezea juu ya Mr kutorudi kwake nyumbani.
Sikia mamii,Usiwe unaniambia mambo ya huyo bedui kabisa. Ninaweza kumfanya kitu mbaya. Please sitaki kusikia anakutesa kabisa. Pole. Ndio maana nipo mimi kuhakisha usalama wako. Na ni kwa vile naogopa tuu kukuambia Uachane naye maana sijajua unamaagano gani na yeye,ila sio mwanaume huyo. Sio kabisa.
Aliniambia naomba nije kukuchukua.
Sawa niliitikia. Hapo nilikuwa nalia sana. Moyo umejaa uchungu na hasira za hali ya juu. Saa nne aliniambia nimkute mahali. Nilifika na atukaondoka. Akinihurumia sana na akaniambia,
Nakuonya mpenzi wangu. Sitaki kusikia juu ya huyo mwanaume akikufanyia unyanyasaji. Sawa mama. Nataka ukikutana na mimi tuongee maisha ya Raha tuuuu. Ufurahie maisha sawa mama. Usilie kabisa. Uko na Real man. Sawa mpenzi. Nyamaza. Nilijifuta machozi. Nikasema jamani mwanaume ndio huyu sasa. Aliniambia nataka tuongie supermarket tununue chakula. Enhe mamsapu,Nitume sasa. Niambie chakula gani unataka nikanunue. Samaki,kuku na kingine?
Nilitabasamu nikamwambia sawa kabisa na beef filet usisahau.
Aliingia supermarket akatoka na mazaga zaga kibao.
Haoo tukaanza safari ya kuelekea BEMBEA LODGE. Bado ninatafakari,Huyo mke ana kasoro gani jamani?Huyo mke mbona haonekani kuwa karibu na huyu mwanaume?
Any way. Atajijua. Hata mimi nimekwapuliwa wangu. Atajijua. Wacha nivute raha zangu.Haoo tuliendesha mpaka tukafika. Tukaingia ndani ya mjengo.
Alitoa mfuko ambao ulikuwa na nguo. Akaniambia mami najua unahofu. Huo mfuko una khanga,na nguo zingine nimekununulia zawadi. Nilitabasamu. Mh.. Nikaguna. Nilichukua na kuangalia. Kulikuwa na nguo blauzi mbili nzuri na Khanga mpya pair 2.
Na nguo za ndani.
Huyu mwanaume ni wa aina gani?Huyu baba jamani katoka wapi?Nilitafakari haraka. Mbona upendo uliokithiri huuu jamani?Dah.
Aliniambia you can change mamii. Chumba hicho hapo. Jiskie huru kabisa.
Na yeye alingia ndani na kuvua nguo alizokuwa kavalia na shati la kadeti ambalo lilikuwa ni uniform ya kazini. Na kuvaa singland na kaptula. Sasa nikaqeza kuona mwili wake barabara ukivyogawanyika.
Akaniambia Go and change,jiskie huru mama yangu. Nami nikaingia ndani na kubadilisha nguo. Khanga moja mamii.. kazi kweli kweli.. Akijisemea. Nilitabasamu na kutoka nami nimebadilisha nguo. E waaaa... sasa Unaonekana mwanamke wa Fadhili sasa. look at you mamii.
Mwanamke hasa. Hivi wanaume wengine wakoje?Mwanamke kama wewe ni adimu sana kuparikana duniani humu dah. Aisee umeumbika hasaa mama.
Ingia jikoni sasa mhudumie mume wako. Kisha nina wageni wangu watakuja kula lunch sawa mamii.
Moyo ukafanya paaaa... Wageni tena?
Ndio. Usiigope. Uko kwenye mikono salama. Usiogope kabisa. Nitakulinda. Nataka penzi letu lidumu milele.
Usiogope kabisa.
Nilijiuliza ni wageni gani? Nikiingia jikoni na kuanza kupika. Nilipika wali na samaki na njegere. Kisha tukatengeneza juice.
Baadaa ya hapo nikaandaa mezani. Akaniambia kaaa hapa mamii upumzike. Sema nikupatie kinywaji gani,Nikamwambia nitakunywa juice.Ok... Yeye akachukua tena pombe yake na kujimiminia na kuanza kunywa.
Muda mwingi alikuwa akiwasiliana na simu za kazini. Akitoa maelekezo kwa wafanyakazi.
Lakini sikuona wala kusikia hata simu moja akiwasilina na mke wake.
Kuna mwanaume natamani sana akuone na mimi. Najua hataamini na aliniapia siwezi kukupata. sasa nataka aje aone kabisa uko na mimi.
Akicheka akagonga na mimi. Kisha akaniambia hao wanakuja,Nilimuuliza ni kina nani na hakusema. Dah. Nilikuwa dirishani nachungulia wakati yeye katoka kwenda kuwapokea. Nilicheka kuona ni Mama Karisa na Mchepuko wake. Nilicheka sana.
Wliingia nikasalimiana nao. Na story zikaanza na tukala.
Japo mama Karisa akionekana hana raha kabisa. Sasa sijui shida ilikuwa wapi. Lakini akionekana sio yule. Nilimuuliza na akaniambia hana neno kabisa.

*************************
Tulikula, Wakunywa wakanywa. Wakulala wakalala. Na baada ya kupumzika Tuliamka na kujiandaa kuondoka . Mungu wangu,Nimezini kwa mara ya kwanza tangu niolewe. Niliwaza sana akilini. Sikuwa na furaha hata kidogo. Moyoni nilisikia majuto. Lakini najikaza tuuu. Fadhili aliniona sina raha. Nina uhakika alijua kabisa nimepata hofu. Lakini pia aliniambia Nisiogope ni mwanzo. Nitazoea tuu. Uwiii. Sikuamini kabisa kama inawezekana mimi siku moja kuzini. Nilipata mawazo sana. Utazoe,Usiogope Mamii. Fadhili alisisitiza.
Nimezini bila kupima afya, Lakini Fadhili he ia health. Ilikuwaje hata nikakubali mimi sijui. Mbwembwe zake ndizo zilinifanya nikajikuta nakubaliana naye tena kwa hiyari kabisa bila kulazimishwa.
Baada ya hapo Tuliondoka. Na sasa nikiondoka na Mama Karisa haoo mpaka nyumbani kwangu. Njiani tuliongea mambo mengi sana ya maisha na ya ndoa. Na aliniashusha nyumbani kisha akaondoka zake akaniacha.
Niliingia ndani ni saa mbili kasoro . Na mr hajarudi. Na hatuwasiliani kabisa na simu.Nilisema na mimi sitampigia. Moyo wangu ukawa unaniuma sana. Hivi kumbe hata ukipata mchepuko bado mume akikosea unaumia ee. Nilijiambia. Nimepata mwanaume,Anayenipenda sana, anayenipa pesa na mapenzi,lakini mbona bado naumia Juu ya mume wangu?Huyu baba Davis jamani mbona harudi nyumbani?'Nilikuwa najiuliza alipo. Niliumia sana nikajikaza tuu.
Asbh niliamka na kujiandaa kwenda kazini. Siku mbili sijaenda kazini. Nilifika kazini nikafanya kazi zangu lakini akili ikiwa inazunguka. Upande huu unawaza penzi jipya. Upande huu inawaza kutendwa na mume. Niliumia sana nikiwa ofcn.Fadhili sio mwanaume wa msg wala kupiga simu kama hutampigia.
Na makubaliano yetu ilikuwa ni kukutana tu kwenye Mjengo wake,BEMBEA LODGE.
nikajiuliza mbona mke wakw haji,nikajua lazima atakuwa aiza ni mwanamke ambaye ni mzembe ama la mume anaweza kuwa hataki mke ajue vitu vyake. Lakini kwenye picha mwanamke anaonekana ni mjanja na mshapu. Any way... Watajijua.
Nikikumbuka Fadhili aliniahidi gari. Nikasema hivi kweli alimaanisha ama ni feki feki tuu?
Nitamkumbusha.
Nimeshaanza kumzoea,natamani hata nionane naye tena. Ni mwanaume wa kunifaaa. Jioni inafika na Sijaongea na Fadhili wala kuonana naye.
Niliamua kumpigia simu.
Nilipiga mara kwa kwanza ikakatwa, nikapiga tena ikakatwa,Nikapiga tena ikakatwa. Badae akaniambia am home honey.... pleasw dont call.
Nikaelewa. Ila nili mmisi. Nikatamani hata angenisalimia.
Baada ya nusu saa nikaona ya nini niteseke,Nikamuandikia msg kwamba ninampenda na nina mmisi. Hakujibu msg.
Na nikaamua kupiga simu. Nilipiga simu yake na alikata na akazima kabisa.
Niliumia sana kwa nini anizimie simu. Nilitamani pakuche ili niongee naye.
Siku zikasonga,sijaonana naye.Nikimuuliza mama Karisa ananiambia he ia busy. Mbona hajaniambia?
Mama Karisa akaniambia mwanamke naona unataka ndoa wewe, Huyo mume wa mtu mama. Tulizana.
Nilikuwa nammisi hasa.Baada ya siku kama nne hivi Akapiga simu na Kuniambia tukutane Bembea Lodge kama kawaida. Yani ilikuwa ni siku ya jumapili wala sikujali. Na mr alikuwepo lakini sikujali. Nilivyo mmiss Fadhili naachaje kwenda. Mr alikuwepo nikamwambia naenda Salon. Akanijibu dry,Sikujali. Huyooo nikaking'oa hadi mahali Pa kukutania.
Nikafika tukakutana na Fadhili nikapanda gari haooo mpaka maskani. Tukikunywa,tukala,tukalala tukaamka.
Nilikunywa sana pombe kwa sababu nilikuwa na.stress za kutosha. Mpaka saa moja ndio nashtuka ,Nakurupuka na kuanza kujiandaaa. Niliangalia simu ya Mr ina missed call kama 20 hivi. Kapiga mpka kashaa. Anajua salon ambayo huwa naenda kila siku. Bila shaka alienda hapo. Maana Dada wa Salon aliniandikia msg na Kusema Mr wako kaja hapa tumjibuje maana atarudi. Akiandika kama msg 10 lakini sikuona. Maana nilikuwa chumbani na Fadhili.
Niliogopa.sana.
Fadhili alikuwa kalewa sana. Alikunywa sana hii siku. Nikamuomba anipeleke akaniambia nimuite Dogo. Dogo akaniambia yuko mbali sana. Hatafika kwa wakati. Nilijiskia kulia. Fadhili alikuwa kweli kachoka sanaa. Nilichukua simu nikampigia mtu wa taksii. Nikamuelekeza na baada ya dakika kama 50 hivi akafika.
Nilichukia sana lakini sikuwa na namna.
Nilipofika home Mr alikuwa ndani. Akanitazama na kuniambia,Mama Davis unanitafutia Mada. Umetoka wapi?Kwa vile nilikuwa na woga nikasingizia vikoba. Anajua napenda vikoba.
Aliniambia bahati yako. Leo nimelala vizuri. Ila naomba tabia za kuja kwangu usiku sitaki kabisa.
Sawa mume wangu. Niliitikia.
Kisha nikamkaribisha mezani. Akaniambia kashiba.
Mh, Niliguna tuu. Nikitamani kujua Fadhili anaendeleaje maana nilimuacha akiwa kalewa na kalala. Nilipiga simu kuona kma atapokea. Iliita sana bila mafanikio.Nikaandika msg,Vipi diaa uko poa?
naomba ukipata msg nipigie.

Loading....



ITAENDELEA SEHEMU YA TANO