NAIPENDA JUMAMOSI YANGU SEHEMU YA 3 - Chumba Cha Mapenzi -->

NAIPENDA JUMAMOSI YANGU SEHEMU YA 3

fb_img_1559779836804-jpg.1119131


Ndo siku ya kwanza naanza kujifunza uchepukaji. Swali langu ni je Mke wa Fadhili yuko wapi?Wanaishije?
Najihoji maswali mengi. Tangu niingie Ndoani kamwe sijawahi kuchepuka. Ama kwa hakika Ndoa huharibu tabia za wanawake. Hivi mume wangu angenipenda haya yangetoka wapi?Potelea mbali.
Atajijua. Na huu ni mwanzo tuu.Nilijikuta namkumbuka tena Fadhili. Na sasa nikampigia Simu kuongea naye. Akapokea na kucheka sana. Akaniuliza Jamaa yako hayuko hapo Karibu?Nikamjibu hayupo. Akaniambia sema mamii. Nikamwambia sina usemi nimekumiss tuu. Akaniambia Nakupenda. Kama vipi Kesho tuonane nikitoka mazoezi. Tuonane mapema.
Mh. Nikamwambia sawa kabisa.
Basi tukaagana. Baada ya muda Mr akaja. Mr nilimwambia nilienda salon. Aliporudi akanitazama na kuniambia mbona hujaenda salon na ulisema uko.salon?Nikamwambia nikiahirisha baada ya simu yako.
Akanitazama akaguna.
"Huo umalaya unaojifunzia uzeeni utakugharimu. Usisahau Condom usije Ukafa"
Mr akaniambia.
Dah. Nikasema ni nini hii lakini?Maneno gani haya?
Sikia Mama Davis. Unaonekana kabisa kuna tabia umeanza. Sitaki mada kesi. Hao mabwana zako kuwa nao makini. Nisije kata shingo yako ama ya mwanaume hapa mjini. Ohoooo... Haya.
Baba Davis aliongea kwa hasira lakini kwa vituo.
Sikujali japo nilikuwa naogopa nikihofia kipigo.
Hembu hiyo simu yako,Baba Davis alisema. Nilichukua simu na kumpatia. Wakati huo nilishafuta calls zoote za Fadhili. Akaangalia kisha akanirudishia simu.
Sikia,Mji wa Arusha mdogo sana. Kwa vile umeamua kufanya ufuska,nikuombe kuwq makini. Sitatamani kukuaibisha.
Alirudia tena.
Nilikuwa tu kimya. Nikajiuliza kukikoni?Amejua ama?Amehisi ama?
Mwisho nikasema potelea mbali. Aniache.
Nikaandaa chakula akasema hatakula. Na akahama chumbani. Akawa analala chumba cha wageni. Mh. Lakini nikasema sawa. Uamuxi ni wa kwake.

*************************************
Mume wangu ni mbabe sana, na siku zote za maisha yetu, tumekuwa ni watu ambao hautuwezi kukaa pamoja na kujadili jambo. Yani akiamua ameamua, hakupi uhuru wa kuchangia mada wala kkutoa wazo. Ninamfahamu. Hivyo hata hapa namuulizaje juu ya kuhama chumba?
Niliamua kumuacha tu. Nakumbuka siku za nyuma sana, aliwahi kuwa na mahusiano na msichana mmoja ambaye alikuwa ni mwanachuo, alikuwa anasoma chuo cha uhasibu. Niliumia sana kipindi hicho, nilipojaribu kumuuliza kulikoni baada ya kuona ticketi mbili xa ndege za kusafiria yakweke na ya huyo dada anaitwa Herieth, nilipomuuliza alinigombeza sana na kunitukana sana, na aliniambia sitamuona nyumbani kwa sababu ana mdomo, mpaka siku nikiacha mdomo ndipo nimuambie aje nyumbani.
Kweli alihama nyumbani kama miezxi miwili hivi, nikajua kabisa anaishina huyo msichana, Mpaka badae Yule msichana alipomaliza chuo na kuondoka ndipo mahusiano yao yakafa, hata hivyo nilipoona kahama nilianza kujibaraguza na kumuambia sitamsemesha tena arudi tu tena anisamehe.
Hivyo nimekuwa nikiteseka sana ndoani hata kumuonya sikuwa nathubutu. Maisha yakawa hivyo.
Sasa leo naanzaje kujadili mada ya kuhama chumba? Yamkini ana mwanamke wake ndio maana kahama.
Lakini na mimi nikasema potelea mbali, maadamu na mimi niko na Fadhili basi wacha ngoma iwe droo. Akidhani kanisusia mimi nakusanya nguvu na mapenzi ya Fadhili. Na sasa nikaamua kabisa wiki hii ni mapenzi moto moto na Fadhili. Na hivi Mama Karisa kashaniambia Niache uzoba, basin a mimi nikasema liwalo na liwe.
Asbh nilijiandaa na kwenda kazini. Nilifika kazini na kufanya kazi haraka haraka, ama kweli Penzi kitovu cha uzembe. Nikasema kwa nini nisiombe ruhusa naenda hata hospital ili nikaonane na Fadhili? Ni mida ya saa nne asbh. Nilianza kuongea na wenzangu kwamba najisikia vibaya, na hivi karibu staff nzxima walikwua wanajua nimepigwa walinihurumia na kuniambia nenda tu mamii. Nilichukua pochi yangu, nikaondoka na kuelekea kwenye mgahawa ambapo nilikaa hapo na kuanza kupiga simu.
Nilipiga simu ya Fadhili na haikupokelewa, niliipiga sana kama dakika kumi hivi bila majibu.
Nikaamua kuagiza supu nikawa nakunywa. Badae Nilisikia simu inaita, niliitoa kwenye pochi na kuitazama, ni Fadhili anapiga, nilitabasamu kwanza kabla ya kuipokea, kisha nikapokea.
Haloo .. … haloo diaaa upande wa pili uliita.
Ni Fadhili aliyekuwa anaonga.
Sijambo, wewe mzima? Nilimuuliza.
Ndio mimi mzima kabisa, alinijibu. Kisha akaniambia , samahani sikuona simu yako, nilikuwa busy na shughuli za hapa na pale.
Pole sana, nilmjibu. Asante akaitika.
Niambie mamsapu… aliniambia.
Nilimwambia nimekumiss tu, niko nimekaa mahali nikaona nikupigie.
… Ha ha ha… Alicheka na kuniambia wewe mwanamke unataka kuniua eeee.. niko kazini, kunashughuli nazifanya hapa, kisha nitatoka saa nane, alafu baada ya hapo nitapitia mazoezini nitatoka saa 12. Ulikuwa unasemaje mamii?
Mh… niliona ratiba yake ilivyokuwa imejaa. Sijui hata anafanya kazi wapi. Kazi ya kutoka saa nane ni kazi gani hiyo? Nilijihoji kisha nikakosa jibu nikanyamaza.
Nilikuwa nimekumiss tu, nimepata nafasi kazini nikasema nikupigie nikidhani uko na muda ili tuonane.
Dah… alisema, kisha akawa kama anataka kusema kitu kwa sekunde kadhaa.. ammmmm… ammm… ngoja kidogo subiri hapo hapo nikujibu.
Fadhili alikuwa anaongea na mtu mwingine na nikawa nasikia…
Imrani hembu niambie ile oda ya Mr Makambi imeshashughulikiwa?
Aliongea hivyo, kisha nikasikia tena akisema, Od azote za jana na juzi zimekamilika, Invoice ziko tayari.
Alipokuwa anaongea hivyo alinirudia na kuniambia, Mamii.. naomba tukutane saa saba, nitamtuma dereva aje akuchukue, unielekeze utakapokuwa. Nilimwambia nitakuwa salon nikitengeneza kucha.
Alimaliza kisha na mimi nikapumua,kwa sababu ukweli nilihitaji faraja na sikutaka kujali inatoka wapi kikubwa ni faraja. Na leo nilipanga nitakuwa na maongezi na Fadhili ya kina, maongezi ambayo yatanipa kumjua yeye vyema, historia yake na familia yake, lakini pia swala la afya yake.
Nilipomaliza kunywa mtori, sikuona sababu ya kurudi kazini kwa sababu nilishaaga, na niliamua kuelekea salon.
Nilifika salon na kuamua kutengeneza kucha za mikononi na miguuni.
Saa saba kamili on dot, Fadhili alinipigia simu na kuniambia, Mamii, Dogo (akimaanisha Dereva) Atakuja kukuchukua hapo salon, Sawa niliitika.
Na baada ya dakika chache sana Dogo alifika, na kunichukua.
Alinisalimia, Dogo ni dereva wake, ni kijana mwenye lafudhi ya Kisambaa, bila shaka ni msambaa huyu. Kijana mweusi na mfupi. Alinisalimia shikamoo Sister, niliitika kisha nikapanda kwenye gari na kuelekea alipoambiwa annipeleke. Nilijua ni kule kule kwa siku zote. Lakini sasa sio huko , niliona kabisa Dogo akiendesha kuelekea sehemu ingine kabisa. Ni nje kidogo ya mji, nilishangaaa.. Tuliendesha kwa dakika kama 30 hivi, ni zaidi ya km 20 kama sio 30.
Aliendelea kuendesha, na sehemu hiyo ilikuwa ni sehemu ambayo hakuna makazi mengi ya watu, nilikuwa nikiona nyumba mbali mbali sana. Na baada ya dakika chache sana tukawa tumefikaa.
Ni eneo zuri na llina jengo jipya sana. Dogo aliniambia hapa ni kwenye mradi wa Bro. Ni hotel anajenga. Hii ni hotel.
Ni sehemu nzuri sana, na Jengo lake kubwa sana, lakini bado halijamalizika. Tulikuwa walinzi na wafanyakazi wengine wakiwa wanajenga na kufanya usafi na kuotesha miti na maua.
Nilipelekwa moja kwa moja kwenye moja ya nyumba ndogo iliyopo ndani ya eneo hilo hilo. Nyumba hii ilikuwa imemalizka vizuri kabisa. Ni nyumba ambayo inazo mpaka na feniture.
Dogo aliniambia nakuacha hapa, Bro anakuja sasa hivi. Nilikuwa naogopa,, hapana Dogo, usiniache peke yangu, ngoja mpaka Fadhili aje. Niliogopa kwa sababu ni sehemu ambayo ni ngeni kwangu, lakini pia ni mbali sana. Niliogopa. Usiogope sister.. Wakati tunaendelea kujadili mara geti kubwa na honi zilikuwa zikipigwa sana, na Dogo akaniambia Broo huyo. Dogo alitoka kwenda kumpokea Bro, na kuniacha ndani.
Fadhili alifika na akawa anazunguka hku na huko kama nusu saa hivi huku akitoa maelekezo na alikuwa kama akilipa watu pesa, na baada ya hapo, alikuja.
Pole mamsapu.. alinikumbatia na kunibusu, Na kuniambia pole nimechelewa,, umeogopa eeee….
Aliuliza… ndio, nimbali sana huku,,, Alitabasamu.. akasema yes. Panafaa sana kupumzika huko , nimejenga hapa kwa ajili ya mapumziko, Ni lodge hii. Imenila sana pesa, na kunisumbua sana akili. Iishe tu.
Alisema Fadhili. Alionekana kweli kama ambaye amechoshwa na jambo.
Hapa kitakachonisumbua ni Umeme, ninapata taabu sana na Umeme, yani nikipata umeme hapa nitafungua hii lodge rasmi mwaka kesho. Ninataka kuifungua mwakani. Lakini umeme utanichelewesha.. Naomba nikuzungushe uone Lodge ya mpenzi wako… Alisema h ivyo kisha akanikumbatia na kunibusu na kuzungusha mkono wake kiunoni na kuchukua wangu na kuuxungusha kiunoni mwake na kuniambia usiogope… mimi ndiye mpenzi wako, Mwanaume wako niliiyeumbwa kwa ajili yako. Usiogope.
Alinishhika kwa ujasiri sana, nikajiuliza jamani huyu kaka ana mapenzi sana, Sijawahi kupendwa hivyo muda mrefu sana.
Mwanaume ambaye ni handsome, ambaye anautunza mwili wake kwa mazoezi, anaonekana mwenye pesa, anaonekana mwenye mapenzi, dah.. kuna wanawake wana bahati duniani sana. Nilitamani kumjua mke wake sa.a
Tulitoka nje na kuanza kutembea, na kuanza kunielekeza na kuniambia kila eneo ni sehemu ya nini na nini. Ni jingo la gorofa 4. Kila floor ina room 8. Room nzuri sana ambazo zimeshamalizika bado finishing kidogo sana.
Baada ya hapo akaniambia hapa ni ukumbi mdogo wa mikutano, utachukua watu 100 mpaka 15 tu.
Na lodge yetu (akasema lodge yetu as if nahusika sanaa, wanaume jamani, Na mimi likichwa linafura kabisa.) Lodge yetu itachukua wateja wa kulala 60 tu kama itakakuwa imejaa, Nataka ya wateja wachache ili wapate huduma amaizing.
Ahaaa… utaitaje? Nilimuuliza,,, Alitabasamu, akaniambia niambie mpenzi niipe jina gani? Nilicheka na kumwambia sina jina mbona, akaniangalia akaniambia nitaiita BEMBEA LODGE . Ama ulitaka niiiteje mamii? Hapana, jina zuri sana.
Aliniambia na hapa ndipo nitajenga swimming pool , na wataanza wiki ijayo kuijenga.
Kisha baada ya hapo akanipeleka kwenye jingo kubwa ambalo ni kama stoor, aliita, Amiri… Amiri alikuja akiwa anakimbia na akafika na funguo, Alifungua mlango na tukaingia ndani. Dah… nilishangaa kuona feniture nzuri sana na nyingi mnoooo, na mabox ya tv, akaniambia mamii, si unaona, hivi vyoote ni vifaa na feniture za lodge yetu, nilishanunua kila kitu, ila kufunga tu sasa ndiyo bado kwa sababu umeme ndio tatizo.
Tulimaliza na kuzunguka kila eneo na tukarudi kwenye ile nyumba nzuri sana ambao ina room 3 za kulala, sebule, dining hall, jikoni na stoor.
Nilikaa Sebuleni ambapo kulikuwa na feniture zoote. Aliniambia mamii nikupikie? Nilicheka, alifungua friji na kutoa sausage pakiti nxzima, na kuzichemsha kwenye jiko la gesi.
Kisha akatoa box la juice kwenye friji, akaleta na glass mbili na kuweka mezani. Na kutoa chupa ya maji ya Kilimanjaro akaweka mezani pia. Tukaanza kula alinikaribisha.
Dah, nilishangaa sana ,
Fadhili, samahani, ninaweza kukuuliza swali? Ndio mamii niulize tu, Aliniambia akionyesha kuwa na shauku ya kutaka kujua namuulixa nini.

ITAENDELEA SEHEMU YA NNE 

FUATILIA POST ZETU KILA SIKU